KATIBA
YA
KIJOGOO GROUP FOR COMMUNITY DEVELOPMENT
KIPENGELE 1. JINA LA SHIRIKA
Jina
la shirika ni Kijogoo Group For Community Development
Kijogoo
Group For Community Development shirika lisilo
la
kiserikali
KIPENGELE 2. SHERIA
2.1
Kijogoo Group
For Community Development ni shirika lisilo
la kiserikali
au (NGO) lililosajiliwa chini Sheria
ya NGO ACT NO- 24/2002
KIPENGELE 3 UTANGULIZI
Shirika la Kijogoo Group For Community Development limeanzishwa kwa kusudi ya kusaidia
jamii kwa kuiweka pamoja kwa minajiri ya kushauriana na kubadirishana mawazo na
uzoefu katika kuyatafuta na kuyasimamia maendeleo katika Nyanja na sekta zote
kwa lengo la kuinua na kukuza uchumi wa watu kwa kuzingatia makundi yote.
Kijogoo Group for Community
Development imeona iko haja ya kufanya ushawishi na uhamasishaji wa jamii ili
ijitambue na kuchukua hatua za kupambana na adui Umasikini kwa kufuata sheria
na miongozo ya nchi ili kuinua hali za maisha za wananchi na utekelezaji wetu
utakua ukiangalia sana vipaumbele vya wananchi wenyewe kulingana na wakati na
mahitaji yao.
Katika kutekeleza majukumu yetu
tutazingatia makundi yote yakiwemo na vijana, watoto,watu wenye
ulemavu,wazee,waishio na vvu/ukimwi,wanawake na hasa waishio katika mazingira
magumu hasa umasikini.
Lengo kuu ni kupambana na
umasikini kupitia shughuli zinazokubalika na jamii na kufuata sheria
inayoelekeza uendeshaji wa mashirika yasiyo ya kiserikali.
Sisi Kijogoo Group For Community Development kwa niaba ya wapenda maendeleo
wote nchini Tanzania kwa nia njema tumeamua kuunda shirika hili na kutumia
katiba hii katika kusimamia haki na kutuongoza ili tusiende kinyume na sheria
inavyo elekeza.
SEHEMU YA PILI
KIPENGELE 4. KUTAJWA KWA KATIBA
4.1 Katiba inatajwa kwa jina la katiba ya Kijogoo Group For Community Development
na itaanza kutumika baada ya kupokelewa na
kukubalika na wanachama katika
mkutano mkuu wa kwanza wa wanachama wote
waanzilishi na baada ya kuwa
imesajiliwa na mamlaka iliyo na uwezo katika Nchi.
KIPENGELE 5. AINA
5.1. Shirika hili
litajulikana kwa namna mbalimbali kama Kijogoo
Group For Community Development.
KIPENGELE 6. USAJILI
6.1. Shirika hili
litasajiliwa na mamlaka yenye uwezo chini ya sheria ya Mashirika
yasiyo ya kiserikali ya mwaka 2002
KIPENGELE 7. MAKAO MAKUU
7.1.Makao makuu ya shirika yatakuwa Morogoro Tanzania bara
7.2.Shirika litafungua matawi katika maeneo mbalimbali nchini
Tanzania kwa kuzingatia
mahitaji.
7.3.Anuani ya shirika itakuwa
Kijogoo
Group For Community Development
S.L.P.
1198, Morogoro,
Simu Na. 0754 948767/ 0715 948797
KIPENGELE 8. LUGHA YA SHIRIKA
8.1 .Lugha zitakazotumika
katika shirika ni
> Kiswahili
> Kiingereza
KIPENGELE 9. MAMBO MUHIMU
9.1. Usawa
9.2. Jinsia
9.3. Unyenyekevu
9.4. Uwazi
SEHEMU YA TATU
KIPENGELE 10. IMANI YETU
10.1.
Kijogoo Group For Community Development
tunaamini kwamba Umasikini unasababisha ukiukwaji wa utawala bora usiozingatia
uwazi ushirikishwaji na uwajibikaji kutokana na kukosekana kwa usawa na fursa
katika uchumi kwa jamii kunapere kea
utamaduni na muundo unaoleta athari kwa makundi hatarishi wa kiwemo wanawake.watoto,wazee,walemavu na
vijana waliopo kati ka maeneo ya
vijijini na mijini
KIPENGELE 11. DIRA
11.1.
Kuona Jamii yenye uelewa wa kufanya ufuatiliaji wa mapato na matumizi ya Rasilimali za Umma
KIPENGELE 12 DHIMA
12,1. Kujenga uwezo wa Wananchi na Viongozi kwa Kuelimisha na kuhamasisha kusimamia na kutekeleza
Sheria,Misingi na Kanuni za utawala unaozingatia uwazi ushirikishwaji na
uwajibikaji katika matumizi mazuri ya
Rasilimali za Umma kwa njia ya mafunzo vyombo
vya habari, vipeperushi, majarida na
mikutano
KIPENGELE 13. MADHUMUNI
13.1.
Kuikusanya jamii na kuwaelimisha kwa kuwapatia mafunzo kwa nadharia na vitendo
kwa kuwapa ujuzi maarifa yatakayowasaidia ka tika kuendesha maisha yao.
13.2. Waweze kupambana na
umasikini kwa njia ya kwa kujituma na kuji saidia wenyewe na kusaidia makundi
mengine lengwa wakiwemo watoto,yatima,vijana wazee,wanawake na walemavu
13.3. Kuanzisha mpango wa elimu kuanzia shule za awali mpaka vyuo
ili kuwapa fursa ya kusoma kwa wale wenye mahitaji hayo
13.4. Kuwaweka vijana kuwa pamoja na kupata fursa ya kujadili mambo
ya kimaendeleo kwa kubadilishana mawazo kama njia moja wapo ya kujifunza.
13.5. Kuihamasisha jamii katika kutunza na kuhifadhi mazingira
13.6. Kupiga vita vitendo vyote vinavyoashiria rushwa katika maeneo
yote yanayotoa huduma za kijamii pamoja
na jamii kuelimishwa juu ya haki zao na
kutambua wajibu wao kwa lengo la kuinua utawala bora kupitia utetezi na njia nyingine ikiwa ni
pamoja na kutafsiri za sheria kwa kuleta uelewa kwa wote
13.7. Wanawake kupewa fursa na kushiriki kikamilifu kwenye shughuli
za kimaendeleo na za uzalishaji mali.
KIPENGELE 14. SHERIA NA UVUJWAJI WA SHERIA
14.1.
Katiba hii sheria na tarabu zilizowekwa chini ya mamlaka yake zita jumuisha utekelezaji wa kifungu cha sheria za
(Sheria ya NGO ACT NO< 24/2002)
au sheria nyingine zozote zenye adhira
kama hizo kuhusu mambo ya jamii kwa jumla kwa utekelezaji wa sheria za
adhabu za jamuhuri ya Muungano wa Tanzania zitahusika popote patakapotakiwa
SEHEMU YA NNE
KIPENGELE 15 .UANACHAMA
Uanachama katika shirika hili la Kijogoo Group For Community Development
uko wazi kwa watu wote wanaotaka kujiunga na shirika bila kujali
rangi,kabila,jinsi,elimu ya mtu wala dini.
KIPENGELE 16. AINA ZA
UANACHAMA
16.1Wanachama
waanzilishi
16.2Wanachama
wanaojiunga baada ya shirika kuanzishwa
16.3Wanachama wa
heshima
KIPENGELE 17. SIFA ZA
UANACHAMA
17.1Uwanachama upo
wazi kwa yeyote aliyetimiza miaka 18 na kuendelea na awe na
akili timamu
17.2Aliyetayari
kujitolea na kulitumikia shirika kwa muda wake wote anapo hitajika
17.3Anaeguswa na
matatizo yaliyomo kwenye jamii
17.4Aliyetayari kujitolea
mali kwa kuisaidia jamii iliyoguswa na tatizo
KIPENGELE 18. MASHARTI NA
MAJUKUMU YA WANACHAMA
18.1.Mwanachama atajaza fomu maalumu ya kuomba uanachama
18.2.Akikubaliwa uwanachama atalazimika kulipa kiingilio na ada ya
uanachama
18.3.Mwanachama atatakiwa luhudhuria mikutano yote ya shirika
inayomuhusu
18.4.Mwanachama lazima aheshimu uongozi uliopo madarakani nakulinda
mali za
shirika
18.5.Mwanachana atatakiwa kutoa ushirikiano kwa uongozi na
wanachama wenzie
KIPENGELE 19. HAKI ZA WANACHAMA
19.1.Mwanachama anayohaki ya kuudhuria vikao
19.2.Mwanachama anahaki ya kuomba na kupatiwa taarif za kiofisi
19.3.Mwanachama ana haki ya kutoa na kupokea maoni kupitia vikaokusaidia
na kusaidiwa anapopatwa na matatizo kwa kupata huduma zitolewazo na shirika kwa
makundi lengwaMwanachama anayohaki kuajiliwa katika shirika kwa nafasi yoyote
ambayo atakuwa na ujuzi nayo.
KIPENGELE 20. UKOMO WA
UANACHAMA
20.1. Kujiudhuru mwenyewe kwa hiyari yake
20.2. Kufukuzwa kwa utovu wa nidhamu kwa kuvunja sheria,masharti au
makosa
makubwa yasiyokubalika na jamii
20.3. Kufariki dunia
KIPENGELE 21 MATAWI YA
SHIRIKA
21.1 Shirka linaweza kufungua matawi popote katika mikoa ya
Tanzania Bara kama
itaonekana kuna haja ya kufanya hivyo kulingana
na ma mahitaji ya shirika.
21.2.Kila tawi litafanya kazi kwa kutumia katiba hii kwa utaratibu
uliopoila watazingatia
mahitaji yao kwa wakati uliopo
21.3.Tawi lolote litakalo omba ruzuku au kupatiwa ruzuku lazima
makao makuu ifahamishwe kuhusiana na hilo na katika maombi ya kuomba ruzuku
mahala popote lazima barua ya utambulisho wa kutambuliwa kwa maombi hayo
itolewe na makao makuu kuthibitisha kuwa maombi hayo yanafahamika na makao
makuu.
21.4.Uongozi wa matawi utachaguliwa kwa kufuata taratibu za katiba
hii na viongozi kutoka makao makuu watakuwa wasimamizi wakuu katika chaguzi
hizo.
21.5.Matawi yote lazima yawe akaunti ya benki kwa benki
watakayokubaliana kwenye vikao vyao,na lazima jinsia izingatiwe katika kuteua
watia saini benki.
21.6.Matawi yote watawasilisha taarifa zao za kila robo mwaka makao
makuu kwa ajili ya kuunganisha taarifa na kuwa kumbukumbu zitakazo saidia
utendaji kazi wa kila siku.
SEHEMU YA TANO
KIPENGELE 22 MUUNDO WA
SHIRIKA
22.1. Kutakuwa na Mkutano mkuu
22.2. Kutakuwa na Bodi ya Shirika
22.3. Kutakuwa na Sekretarieti
22.4. Mwenyekiti
22.5. Mkurugenzi
22.6. Mtunza hazina
22.7. Afisa Miradi
22.8. Afisa ufuatiliaji na Tathmnini
KIPENGELE 23. VIONGOZI WA
SHIRIKA
23.1.Viongozi wote wa shirika kuanzia mwenyekiti,Mkurugenzi,mwekahazina na
afisa miradi watachaguliwa na mkutano mkuu isipokuwa nafasi ya Afisa
Ufuatiliaji na Tathmini itateuliwa kulingana na sifa na utaalamu.
23.2.Viongozi wote watakaa madarakani kwa muda wa miaka 5 na wanaweza
kuchaguliwa tena kwa kipindi kingine cha miaka 5 (miongo 2) baada ya hapo
anaweza kuchaguliwa kwa kubadilisha nafasi ya uongozi
KIPENGELE 24. MWENYEKITI
24.1. Atachaguliwa na mkutano
mkuu na ataongoza vikao vyote
24.2. Atasaini mikataba yote
shirika ya ndani na nje
24.3. Ndiye msimamizi mkuu wa
shirika
24.4. Ataongoza mikutano yote ya
shirika
24.5. Atakuwa na mamlaka ya kuidhinisha
wa malipo na mdhibiti mkuu wa mapato ya
shirika
24.6. Atawajibika kwenye Bodi na Mkutano Mkuu
KIPENGELE 25. MKURUGENZI
25.1.Atakuwa afisa mtendaji mkuu wa shirika na ndiye katibu katika
vikao vyote
25.2.Atakuwa msemaji na mtendaji mkuu wa shughuli za kila siku za
shirika
25,3.Msimamizi mkuu wa shughuli za kila siku za kila idara shirika
25.4. Atatafuta vyanzo vya mapato miradi ya kuelimisha na ya
uzalishaji mali.kwa jamii
25.5 Atapitia na kuandaa mikataba itakayoingiwa na shirika kati ya
shirika na wafadhili
au shirika na watoa huduma ndani ya
shirika na wanaotoka nje
25.6 Atasaini mikataba yote ya shirika baada ya kujiridhisha
25.7 Ataidhinisha malipo yote yatakayoitahijika kulipwa baada ya
kujiridhisha
KIPENGELE 26. MWEKA HAZINA
26.1. Atachaguliwa na mkutano mkuu
26.2. Atashughulikia maswala yote ya fedha na kutunza vitabu vya
fedha na daftari la
mali za kudumu za shirika
26.3. Awe mbunifu na uwezo wa maswala ya kifedha
26.4. Ataandaa Hati za malipo na kufanya malipo baada ya hati ya
malipo kuidhinishwa
na mkurugenzi ama atakae kaimu
26.5. Atafuata mwongozo wa fedha unavyoelekeza katika kutimiza
majukumu yake
26.6 Atawajibika kwa
Mkurugenzi
KIPENGELE 27 AFISA
UFUATILIAJI NA TATHMINI
27.1.Atachaguliwa ama kuteuliwa na mkutano mkuu baada ya bodi
kuridhia
mapendekezo ya sekretarieti.
27.2.Atashughulikia maswala yote ya utafiti,ufuatiliaji na Tathmini
27.3.Ataandaa fomu /dodoso za zitakazotumika kwenye ufuatiliaji na
Tathmini
27.4.Atatunza taarifa zote zitokanazo na Ufuatiliaji na Tathmini
27.5.Atamshauri Mkurugenzi njia na mbinu ya kupata matokeo na Atawajibika
kwa
Mkurugenzi
KIPENGELE 28. AFISA MIRADI
28.1.Atachaguliwa ama kuteuliwa na Mkutano mkuu baada ya Bodi kuridhia
mapendekezo ya sekretarieti.
28.2.Atakuwa na kazi ya kuandaa maandiko ya miradi na kuiwasilisha
kwa Wafadhili na
wahisani kutafuta ruzuku na misaada ya kuwezesha kutekeleza Miradi ya kijamii
28.3.Atatafuta wafadhili wa ndani na nje
28.4.Ataandaa,kutekeleza,kusimamia miradi yote itakayoteke lezwa na shirka
28.5.Atandaa taarifa zote za utekelezaji wa mradi,matokeo ya mradi
ulio tekelezwa kwa
kupitia taarifa ya ufuatiliaji baada ya
utekelezaji na kuziwasilisha kwa Mkurugenzi
28.6.Atawajibika kwa Mkurugenzi
SEHEMU YA SITA
KIPENGELE 29. VIKAO
29.1MKUTANO MKUU
29.1.Kutakuwa na mkutano mkuu wa shirika wa wanachama wote wakiwemo
waanzilishi Viongozi na Wawakilishi toka katika matawi yetu yote
yaliyofunguliwa maeneo mbalimbali.
KIPENGELE 30. KAZI YA
MKUTANO MKUU
30.1.Kuchagua viongozi wa shirika na kupitisha majina ya wajumbe wa
Bodi na kuridhia mapendekezo ya Bodi kuhusu nafasi za watendaji waliotajwa
kwenye katiba hii ambo watakuwa ni wajumbe wa sekretarieti (Wakuu wa Idara )
30.2. Itapitisha mpango Mkakati wa miaka mitatu, Mpango kazi wa mwaka
na Bajeti shirika kwa mwaka unaofuata au inategemea
maamuzi ya wanachama kulingana mazingira ya kazi yanavyoonekana
30.3. Itajadili na kupitisha/kuthibitisha majina ya wanachama wapya
30.4. Kupokea taarifa ya kazi ya mwaka zilizofanywa na shirika
ikiwemo taarifa za fedha
na za utekelezaji
30.5.Kusimamia maadili na kupokea mapendekezo ya Bodi juu ya adhabu
kwa wanachama wenao kutwa na makosa
KIPENGELE 31. SEKRETARIETI
31.1.Kutakuwa na Sekretarieti ya shirika ambayo itakuwa na jukumu
la kusimamia kazi za kila siku za shirika,idadi ya wajumbe ni 5 ambao wane ni
viongozi waliochaguliwa na mmoja kutoka miongoni mwa wanachama
KIPENGELE 32. KAZI ZA
SEKRETARIETI
32.1.Kusimamia na kutekeleza kazi za kila siku za shirka wakiongozwa
na Mkurugenzi mtendaji
32.2.Kuandaa na kupitia ripoti za kila idara kwa kazi zinazofanywa
kila siku na kuboresha pale panapoonekana kuna haja ya kufanya hivyo.
32.3.Kuandaa rasimu ya mpango wa kazi wa shirika na rasimu ya bajeti
ya kila mwaka na kuiwasilisha kwenye bodi kwa mapitio,maboresho au marekebisho
na kupelekwa kwenye mkutano mkuu kwa kuidhinishwa.
32.4.Kufanya marejea kulingana na mwongozo wa fedha na bajeti
elekezi iliyopitishwa kila baada ya miezi mitatu na kuwasilisha mapendekezo
kwenye Bodi
KIPENGELE 33. BODI YA
WADHAMIN
33.1.Kutakuwa na Bodi ya wadhamini ya shirika itakayoteuliwa na
Sekretarieti na kupitishwa na mkutano mkuu na wajumbe wake watakuwa watu wenye uwezo wa kifikra,
kuheshimika na wenye maadili mema kwa
jamii
KIPENGELE 34. KAZI ZA BODI YA
SHIRIKA
34.1. Kuwa chanzo cha mapato kwa kutafuta wafadhili na wahisani wa
ndani na nje wa kuwezesha utekelezaji wa miradi
34.2.Kuangalia mwenendo wa uendeshaji wa shirika kuanzia kazi na
majukumu wa watumishi hadi maadili kwa
wanachama.
34.3.Kupitia rasimu zote ikiwemo za Mpango Mkakati,Mpango kazi na
rasimu ya bajeti inayoandaliwa na
sekretarieti kwa maboresho na kuiwasilisha kwenye mkutano mkuu kwa ajili ya
kuidhinishwa.
34.4.Kuushauri uongozi chini ya Mkurugenzi na idara zake namna bora
ya uendehaji wa shirika ili kuleta tija na ufanisi wa kazi.
34.5.Itakuna mara 2 kwa mwaka kwa ajili kufanya vikao vyao ila
inaweza kukutana kwa vikao dharula muda na wakati wowote na itachagua
mwenyekiti kutoka miongoni mwao na Mkurugenzi na Mwenyekiti wa shirika wanaingia
moja kwa moja.
KIPENGELE 35. MKUTANO MKUU WA
MWAKA
35.1.Mkutano mkuu wa mwaka wa shirika ndicho chombo kikubwa cha maamuzi
chenye mamlaka ya kupitisha na kuidhisha kutumika kwa sera,Mipango na Bajeti kama katiba hii
ilivyotafsiriwa
35.2.Utakuwa na mamlaka ya kuamua maswala yote yatakayoletwa na Bodi,Sekretarieti
na Wanachama au mwachama yoyote washirika au mjumbe wa bodi kulingana na
taratibu zilizoelezwa kwenye katiba hii
35.3.Mkutano mkuu wa mwaka utakuwa ukifanyika kati desmba na
januari ya mwaka unaofuata
35.4.Agenda za mkutano mkuu zitatokana na kikao cha Sekretarieti na
kugawiwa kwa wanachama wote mwezi mmoja kabla ya mkutano kupitia na kuingiza
maoni mapya yatayozungumzwa kwenye mku tano
35.5.Itatoa taarifa ndani ya siku 21 kwa kubandikwa kwenye mbao za
mata ngazo na kuzisambaza kwa wanachama wote kwa maandishi kueleza tarehe na
mahali patakapofanyika mkutano na agenda za mkutano mkuu na shughuli za mkutano
mkuuzitakuwa ni zile zilizotajwa kwenye agenda
KIPENGELE 36. VIKAO VYA SEKRETARIETI
36.1. Vikao vya Sekretarieti vitakutana mara moja kila baada ya miezi mitatu
36.2. Itatekeleza majukumu yake kama ilivyoelekezwa kwenywe katiba
hii
36.3. Itashughulikia mambo yote ambayo yanahitajika kuangaliwa
baada ya Bodi na
mkutano mkuu kutoa maagizo kwenye
Vikao vyake.
36.4. Itakuwa na taarifa ya
siku 14 kwa wajumbe wa mkutano mkuu
36.5. Itafanya vikao vya dharula pale itakapoamuliwa kufanya hivyo
KIPENGELE 37. MKUTANO MKUU WA DHARURA
37.1.Kutakuwa na mkutano mkuu maalumu utakaohitishwa kwa kutoa
Taarifa ya dharura kwa wanachama wote kwa kuhudhuria kutokana Na udharura wake
kama inavyoelezwa na katiba hii.
37.2.Itafanya marejeo kupitia Mipango iliyopo,Sera,Kanuni na Bajeti
baada ya kupokea taarifa ya utendakazi mbovu wa wakuu wa idara katika kutimiza
majukumu yake ili kurekebisha kasoro zinazojitokeza kabla mambo hayaja haribika
zaidi na kuchukua hatua zinazo stahiki ili kurudisha ubora na ufanisi wa kazi.
37.3.Kuchukua hatua za haraka pindi itakapo pokea taarifa zisizo za
kawaida za mwanachama kutoka bodi na kuchukua hatua kabla ya kusubiri mkutano
mkuu wa mwaka.
37.4.Kujadili kwa kina taarifa za mfadhili anyetaka kulifadhili
shirika kwa kutoa ruzuku ikiwa ni pamoja na kupokea taarifa za upokeaji wa
ruzuku na namna ambavyo Uongozi ulivyoingia mkataba/mikataba,ili nalo
litafanyika mapema tu baada ya kufanikiwa kupata ruzuku na haitosubiri hadi
mkutano mkuu wa mwaka uitishwe.
SEHEMU YA SABA
KIPENGELE 38. USIMAMIZI WA
FEDHA NA MWAKA WA FEDHA
38.1.Mwaka wa fedha wa shirika la Kijogoo Group For Community Development utaanzia januari na kuishia tarehe 31 desemba
kila mwaka (miezi kumi na mbili)
KIPENGELE 39. VYANZO VYA
FEDHA
39.1.Mapato ya shirika yatatokana na ada za mwaka za
wanachama,viingilio vya wanachama.
39.2.Ruzuku kutoka Taasisi za ndani na nje,kupewa na
wahisani,misaada,kuchangishana wanachama,zawadi,kutoka kwa watu binafsi,taasisi
za ndani na nje ya nchi.
KIPENGELE 40. MATUMIZI YA
FEDHA
40.1.Kulipia kodi za ofisi,kulipia maji na umeme na kununulia vifaa na samani za ofisi pamoja na
kununulia shajala za ofisi.
40.2.Kugharamia mafunzo
mbalimbali ya kuwajengea uwezo wananchi katika mipango,kusimamia na kufuatilia
matumizi ya rasilimali katika kuitekeleza miradi ya maendeleo kwenye maeneo
yao
40.3.Kufuatilia shughuli zilizotekelezwa na kufanya vikao vya
Tathmini kupima matokeo kwa shughuli za miradi iliyotekelezwa kwa jamii Ili kuona hali ya tatizo ya tatizo lililoshughulikiwa
ndani na baada ya utekelezaji wa mradi/miradi.
KIPENGELE 41. FEDHA
41.1 Mapato yote ya shirika yatapelekwa benki kwa hifadhi kwenye
akaunti ya shirika ambayo itaendeshwa kwa saini tatu na mbili kati ya hizo zitatoa fedha benki kwa akaunti ya saving na
kusaini hundi.
41.2 Mwekahazina atatoa taarifa ya fedha zilizopo kwa Sekretarieti
na Sekretarieti itaanda taarifa hiyo na kuiwasilisha kwenye Bodi kwa mapitio na
kisha kurudishwa kwa Mkurugenzi kwa matumizi. na malipo yote yatalipwa kwa
kutumia fomu ya Hati ya malipo iliyoandaliwa na mwekahazina na kupitishwa na mkuu
wa idara na kuidhinishwa na Mkurugenzi au
Mwenyekiti au yoyote aliyekaimu nafasi ya Mkurugenzi.
41.3 Kutakuwa na ukaguzi wa fedha za shirika kwa kila mwaka kwa
kuanda liwa na Sekretarieti na taarifa hiyo ya ukaguzi itawasilishwa kwenye Bodi
na bodi itaipitia kuona kama iko sawa tayari kwa ukaguzi na itapendekeza
mkaguzi wa kukagua mahesabu na kuiwasilisha kwenye mkutano mkuu kwa kupata
idhini na Baraka na kupitia hilo mweka hazina atalazimika kutunza vitabu vyote
vya fedha zikionyesha zilivyopokelewa na
kutumika pamoja na vocha zote za malipo pamoja na vitabu vya risiti
KIPENGELE 42. RIPOTI YA
UKAGUZI
42.1 Mkutano mkuu utaamua kuhusu mkaguzi wa hesabu za shirika
baadaya Sekretarieti kuwasilisha majina ya wakaguzi wenye sifa kwa Bodi na bodi
kupeleka mapendekezo hayo kwenye mkutano mkuu.
42.2 Maelezo ya mapato
42.3 Mizania
42.4 Mabadiliko katika usemi
42.5 Maelezo ya hali ya kifedha
42.6 Maelezo ya mtililiko wa fedha tasilimu
42.7 Pamoja na ripoti ya ukaguzi na uchunguzi wa utendaji ,bodi ya
Wadhamini ya Kijogoo Group For Community
Development itakuwa na utaratibu wa kufanya
ukaguzi wa Muda maalumu kwa uongozi kwa
kufanya marejeo ya miongozo,sera na Bajeti kuhusu taratibu za utendaji kwa
kuzuia kuendelea kwa mapungufu yoyote yanayoweza kutokea kwa kuonekana mapema
katika kipindi cha mwaka
42.8. Baada ya kukamilika kwa ukaguzi na taarifa ikiletwa ofisi
sekretarieti itaipitia na kuiwasilisha kwenye bodi na bodi baada ya kupokea
itaipitia na kuiwasilisha kwenye mkutano mkuu wa wanachama ili waipitie na kama
kulikuwa na mapendekezo yoyote kuhusu ripoti hiyo mkutano mkuu utaamua ya
utekelezaji wa mapendekezo yaliyotokana na dosari au changamoto inayopelekea kushuka
kwa ufanisi katika matumizi ya fedha au kama haijalidhishwa na mkaguzi aliyendekezwa
kufanya kazi hiyo kwa kuwa haina ubora unaotakikana.
42.9. Na ikitokea mkutano mkuu haijaridhiwa na taarifa iliyotolewa
na mkaguzi wa hesabu inaweza kuzipeleka hesabu hizo kwa mkaguzi mwingine kama
kutakuwepo na fedha ya kufanyia shughuli hiyo
SEHEMU YA NANE
KIPENGELE 43. MAREKEBISHO YA KATIBA,KUVUNJIKA KWA SHIRIKA
·
MAREKEBISHO
YA KATIBA
43.1. Katiba itarekebishwa na mkutano mkuu ikifuatiwa na taarifa ya
siku ishirini na moja (21) kwa kusudi la kufanya marekebisho ya katiba itakayotolewa
kwa wanachama Taarifa lazima ijumuishe marekebisho maalumu ambayo yatasomwa na
kujadiliwa sana na wanachama kabla ya kufanyika mkutano wa marekebisho.
43.2. Koramu ya wajumbe wa mkutano mkuu watakao pitisha mabadiliko ya
katiba lazima iwe mbili ya tatu( 2/3 ) ya wanachama wote.
.
43.3. Maamuzi ya kurekebisha katiba yatakuwa halali kwa kwa kuungwa
mkono na robo tatu ya ( 3/4
) ya wanachama wote.
·
KUVUNJIKA SHIRIKA
43.4. Shirika hili linaweza kuvunjika kwa hiyari na
kwa maamuzi yatakayo pitishwa kwa pamojana theluthi mbili ya wajumbe wote katika
mkutano mkuu utakaoitishwa kwa kusudi hili.
43.5 Taarifa juu ya mkutano huu itatolewa kwa wanachama wote ndani
ya siku ishirini na moja(21)kabla ya tarehe ya mkutano mkuu.
43.6 Uamuzi wa kuvunja shirika utakuwa umepitiwa na bodi ya
wadhamini ya shirika na kuteua mufilisi
na itatoa ya kuhusu mali za shirika na namna ya kulipa madeni ya ndani na nje
ya shirika kama yapo.
43.7.Baada ya kulipa madeni yote kama yapo mali zilizobaki zitagawanywa
kwa mashirika ya kijamii yenye malengo yanayofanana na sheria,taratibu
zilizowekwa chini ya sheria ya mashirika yasiyo yakiserikali (NGO) ya mwaka
2002
·
MUHURI WA
SHIRIKA
43.8. Muhuri wa shirika hili utakuwa ni Kijogoo Group For Community Development.
43.9 Muhuri ni nyaraka nyeti utahifadhiwa chini ya ulinzi wa Mkurugenzi
kwa muda
wote.
43.10 Muundo wa muuri wa shirika utakuwa wa duara au yai kimaumbile
kutokana na
mapenzi ya wanachama
SEHEMU YA TISA
44.0 UMUHIMU WA URASIMISHAJI
JINSIA KATIKA PROGRAM
ZA ASASI.
44.1.Kuongeza
ushiriki na ushirikishwaji wa wanawake na makundi mengine ya pembezoni katika
utekelezaji wa program za ndani ya asasi na nje ya Asasi.
44.2.Kuimarisha
usawa na uwiano wa mgawanyo wa majukumu ndani na nje ya Asasi.
44.3.Kuongeza
fursa za uongozi kwa wanawake wanachama wa Asasi.
44.4.Kuimarisha
utetezi wa haki za mwanamke na makundi ya pembezoni.
44.5.Kuongeza
ufanisi na tija katika utekelezaji wa program za Asasi.
44.6.Kuwa na
utaratibu maalum wa ndani ya asasi wa namna ya kupambana na na changamoto za
ukiukwaji wa haki za kijinsia katika utekelezaji wa program za Asasi na namna
ya kuzitatua.
45.0 UMUHIMU WA KUWA NA SERA/MWONGOZO WA FEDHA KATIKA
PROGRAM ZA ASASI.
45.1. Sera za usimamizi wa fedha(Financial Management Policy) katika
Asasi hii kimsingi ni mwongozo unaojumuisha sera za kihasibu ,mifumo pamoja na
taratibu zote zinazozingatiwa katika kutunza na kusimamia fedha za Asasi.Mwongozo
huo unatengenezwa kwa ajili ya kusimamia fedha za asasi na kuwaelekeza
wafanyakazi taratibu zinazopaswa kufuatwa wakati wa kufanya miamala ya fedha
katika Asasi.Lakini pia kuwezesha asasi kukidhi matakwa ya sheria na taratibu
za nchi pamoja na kudhiirisha kuwa Asasi ina mfumo bora na thabiti ya kiuongozi.
46.0. UMUHIMU WA KUWA NA SERA YA AJIRA KATIKA PROGRAM ZA
ASASI.
46.1. Lengo la kuwa na Sera hii ya ajira ni kuongoza katika maswala
mazima ya yanayohusu ajira kwa kuwa na mfumo wa kisheria utakaosaidia kuleta
mahusiano ya ajira yaliyo bora,ya usawa na yenye viwango sahihi vya misingi ya
kazi na pia kuweka mfumo wa kutatua migogoro ya ajira kwa njia ya usuluhishi na
upatanishi na kumfanya kila mfanyakazi kuwajibika ipasavyo katika nafasi yake.
KIPENGELE 47.
MCHANGANYIKO WA MADARAKA
47.1..Kuwekana sawa endapo itatokea hali ya kutoelewana(malumbano)
47.2.Mlalmikaji hatokuwa mjumbe
47.3.Bodi itahusika katika kulisimamia hilo
47.4.Mlalamikaji lazima aikubali kamati ya usuluhishi
47.5.Waamuzi wa migogoro watazingatia vipengele vya sheria za jamuhuri
ya muungano
wa Tanzania.
47.6.Tafsiri ni chombo cha juu kwa kusudi la kutafsiri vipengele
vya sheria hii kitakuwa
ni bodi ya wadhamini.
.
*********************MWISHO****************************
SEHEMU YA KUMI
KIPENGELE 48. KUKILI
48.1.Sisi ni mkusanyiko wa watu mbalimbali ambao majina yetu na
saini zetu zimeonyeshwa ikiwa ni wanachama waanzilishi tunatambua kuwepo katika
shirika hili kwa kufuata katiba kama ilivyotolewa.
NA.
|
JINA LA MWANACHAMA/ANUANI/SIMU
|
SAINI
|
1
|
AMIRI DOTTO
|
|
2
|
RUKIA SELEMANI
|
|
3
|
RAMADHAN SAIDI
|
|
4
|
SADA JUMA
|
|
5
|
TADEI HAFIGWA
|
|
6
|
ADHA KASIMU
|
|
7
|
AGNES HAULE
|
|
8
|
MWAJUMA JULIUS
|
|
9
|
SAIDI DUDU
|
|
10
|
SALUMU OMARY
|
|
11
|
MWAGAIANI AMIRY
|
|
12
|
ALLY KIZIGO
|
|
13
|
MARIAM MAMBO
|
Hongereni sana
ReplyDelete